Friday, 6 March 2015


Home » Ent. » 255 ya March 6, msanii TID, Niki Wa Pili na bodigadi wa Diamond Mwarabu Suleimani wamehusika.

January Makamba - Tanzania Mpya

255 ya March 6, msanii TID, Niki Wa Pili na bodigadi wa Diamond Mwarabu Suleimani wamehusika.

entertainment_news_stopimageInfo ya kwanza kusikika kwenye 255 ya March 6, ni  ishu ya bodigadi wa msanii Diamond Plutnamz anaefahamika kama Mwarabu Suleimani ambae alikuwa Tajikistani kushiriki kwenye mashindano ya kupigana ya Wrestling ambayo yalikuwa na washiriki kutoka mataifa mbalimbali.
LIVINGSTONE MKOI (3) (2)Mwarabu amesema mchezo wa kwanza alicheza na Muitaliano na game ya pili alicheza na Muiran lakini matokeo hayakuwa mabaya tofauti na alivyotegemea lakini siku mbili kabla ya pambano la mwisho alipata jeraha mguuni wakati akifanya mazoezi na kupoteza michezo miwili.
tid4Weekend hii msanii TID kwa kushirikiana na Rader Entertainment pamoja na msanii Nazizi kutoka Kenya watafanya show Bilz, akizungumza kwenye 255 TID amesema amejipanga vema kwa kuwa ni show yake ya kwanza mwaka huu na kutakuwa na wasanii mabalimbali pamoja na surprise za kutosha sambamba na uzinduzi wa video ya msanii Masai Sharo.
nikiStory ya mwisho kusikika inahusu uzinduzi uliofanyika jana wa program mpya chini ya msimamizi wa hati miliki wa Afrika Mashariki (East African Copyright Management) ambapo mgeni rasmi alikuwa Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, January Makamba inayohusu wasanii kulipwa na vyombo vya habari vinavyocheza kazi zao, msanii Niki Wa Pili ni miongoni mwa sananii waliohudhuria ambae amesema itasaidia msanii kupata matunda ya kazi anayoifanya.

No comments:

Post a Comment